BERLIN: Hakuna maafikiano kuhusu tarehe mpya
17 Januari 2007Matangazo
Mpatanishi mkuu wa Marekani,Christopher Hill alikuwa na mazungumzo yasio rasmi pamoja na naibu waziri wa kigeni wa Korea ya Kaskazini,Kim Kye Gwan katika mji mkuu wa Ujerumani,Berlin kuhusika na mradi wa nuklia wa Korea ya Kaskazini.Lakini hakuna maafikiano yaliopatikana juu ya tarehe mpya ya kuendelea na majadiliano ya pande sita kuhusu mradi wa nuklia wa Korea ya Kaskazini uliozusha mabishano.Duru ya mwisho ya majadiliano kuhusu mradi wa nuklia wa Pyongyang ilikuwa mwezi wa Desemba.Majadiliano hayo yalimalizika bila ya kupatikana maendeleo yo yote.