1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Berlin. Aliyejaribu kumuua Hitler akumbukwa.

16 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CI1j

Katika sherehe maalum mjini Berlin, waziri wa ulinzi wa Ujerumani Franz Josef Jung ameadhimisha miaka 100 ya kuzaliwa kwa Claus Schenk von Stauffenberg, afisa wa jeshi la Ujerumani , ambaye alijaribu kumuua kiongozi wa wanazi Adolf Hittler wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia. Jung amekitaja kitendo cha jaribio la kumuua Hitler , tukio la ukombozi, na kusema kuwa von Stauffenberg alikuwa mfano kwa majeshi ya Ujerumani. Mwanahistoria wa Ujerumani , hata hivyo, ameonya dhidi ya kumfanya von Stauffenberg kuwa shujaa wakati alikuwa akiunga mkono malengo ya utawala wa Wanazi kwa miaka kadha kabla ya kugeuka.