1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIJING: Rais wa Ufaransa Jacques Chirac ziarani China

25 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CCzL

Rais wa Ufaransa, Jaques Chirac, amewasili leo mjini Beijing China kwa ziara rasmi ya siku nne inayotarajiwa kuboresha mahusiano kati ya China na Ufaransa.

Rais Chirac anatarajiwa kuzungumzia mzozo wa nyuklia wa Korea Kaskazini na kuitaka China ilishughulikie swala la haki za binadamu.

Rais Chirac ameandamana na viongozi 30 wa viwanda na wanataraji kusaini mikataba ya kibiashara ikiwa ni pamoja na mkataba wa kampuni ya Airbus na kampuni ya Alstom kuiuzia China treni 500.