Katika barua ya mwezi huu, mwandishi wetu Anaclet Rwegayura, anasema karibu kila siku vyombo vya habari vya Tanzania huwa na taarifa zisizoisha za malalamiko ya umma kuhusu masuala mbalimbali, zikiashiria kuwa haki za watu kuwa na maisha yenye hadhi, mafanikio na uhuru zinavunjwa. Anataka ufanisi wa serikali ukomeshe malalamiko hayo.