BAGHDAD:11 wauwawa Iraq
12 Julai 2007Matangazo
Watu 11 wameuwawa magharibi mwa Iraq katika mji wa Karmah baada ya wapiganaji kuwakusanya watu hao ndani ya nyumba moja na kuiripua.Jeshi la Marekani linasema hatua hiyo huenda imechukuliwa na wapiganaji kulipiza kisasi dhidi ya wakaazi wa eneo hilo wanaunga mkono wanajeshi.
Tukio hilo limefanyika kwenye mkoa wa Anbar unaokaliwa na idadi kubwa ya wasunni ambako pia ni ngome ya wasunni wanaopinga uvamizi wa Marekani tangu kuangushwa utawala wa Saddam Hussein mwaka 2003.
Kwengineko nchini humo wizara ya mambo ya ndani imearifu kuwa vikosi vya usalama vya Iraq vimekamata mikanda 200 ya mabomu ya kujitoa muhanga na miripuko mingine ndani ya lori moja lililoingia Iraq kutoka Syria.