BAGHDAD: Wanamgambo wanaimarisha mashambulizi Irak
16 Septemba 2007Matangazo
Watu wasiopungua 15 wameuawa Jumapili katika mapigano na mashambulizi ya bomu,nchini Irak. Tangu kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani,idadi ya vifo vilivyosababishwa na machafuko,imefikia 44.Kundi la “Islamic State of Iraq“ lenye uhusiano na Al-Qaeda limeonya kuwa litafanya mashambulio mapya wakati wa mfungo mtukufu wa Ramadhan.Vile vile kundi hilo limeonya kuwa litawalenga viongozi wa Kisunni wanaounga mkono vikosi vya Kimarekani nchini Irak.