ATHENS: Wapigakura Ugiriki wachagua bunge jipya
16 Septemba 2007Matangazo
Kiasi ya Wagiriki milioni 10 hii leo wanapiga kura kuchagua bunge jipya.Uchaguzi huu uliitishwa mapema na Waziri Mkuu Costas Karamanlis mwanzoni mwa mwezi wa Agosti,wakati ambapo chama chake cha kihafidhina „New Democracy Party“ kilikuwa kikiongoza.
Lakini uchunguzi wa maoni unaonyesha kuwa uchaguzi wa leo utakuwa mchuano mkali kati ya serikali na chama cha upinzani cha wasoshalisti PASOK,baada ya serikali kulaumiwa uongozi mbaya wakati wa maafa ya moto hivi karibuni.