71 wauwawa Somalia
21 Aprili 2007Matangazo
HABARI KAMILI:
MOGADISHU:
Mashambulio ya mizinga katika mji mkuu wa Somalia-Mogadishu yameua hadi leo wasomali 73 huku mamia yakiuhama mji mkuu huo.
Jeshi la Ethiopia linaloisaidia serikali ya mpito ya Somalia imefyatua mizinga na makombora kutoka qasri la rais kusini mwa Mogadishu upande wa vituo kadhaa vya waasi wa kiislamu.Hii ikasababisha jibu kali la hujuma za waasi hao.
Hapo alhamisi Umoja wa Mataifa ulionya kuzuka msiba mkubwa wa wanadamu nchini Somalia huku maiti zikiozeana majiani mjini Mogadishu.Usiku mzima mapigano yakiendelea .