Mazungumzo ya kitaifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kati ya serikali na upinzani yaliyokuwa yatiwe saini jana usiku yamekwama, huku Kanisa Katoliki likitangaza kujiondoa kuwa mpatanishi katika mazungumzo hayo// Mwanaharakati mashuhuri wa Afrika Kusini aliyepambana dhidi ya siasa za ubaguzi wa rangi na mtengano-Apartheid, Ahmed Kathrada, amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 87.