Wanaharakati wa kutetea haki za binaadamu wanasema viongozi wa dunia walionywa kuhusu kuwepo kwa biashara ya utumwa nchini Libya miezi kadhaa iliyopita, lakini walipuuza, na kwa hivyo viongozi hao nao wanapaswa kulaumiwa kwa kile kinachopigiwa kelele sasa ulimwenguni kuhusu biashara hiyo katika taifa hilo lililosambaratishwa kwa vita kaskazini mwa Afrika.