Uingereza itakuwa na kikao cha dharula leo kuhusiana na tukio la kupewa sumu jasusi wa zamani wa Urusi katika ardhi ya Uingereza baada ya Marekani na Jumuiya ya kujihami ya NATO kuunga mkono madai ya Uingereza ya kuihusisha Urusi na jaribio hilo la mauaji// Vikosi vya jeshi la Uturuki vinaripotiwa kuuzingira mji wa Afrin pamoja na vijiji 90, vikiwa na watu wapatao 700,000 nchini Syria.