Nchi za G20 zafanikiwa kuepusha vita vya maneno na Rais Donald Trump kuhusiana na suala la mabadiliko ya tabianchi, mfungwa maarufu wa kisiasa nchini Venezuela Leopoldo Lopez aapa kuendeleza mapambano ya uhuru, baada ya kuachiwa jana kutoka kizuizini na Mkuu wa tume ya uchaguzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo asema haitawezekana kuandaa uchaguzi wa Rais ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.