Chama tawala nchini Afrika Kusini cha African National Congress, ANC, kinajaribu kujinusuru na mgawanyiko uliokikumba baada ya hii leo kutoa wito wa wanachama wake kumuunga mkono Rais Jacob Zuma anayekabiliwa na shinikizo la kutakiwa kujiuzulu// Mataifa yameahidi takriban dola bilioni 1.73 katika msaada mpya kwa Syria wakati wa mkutano wa kimataifa uliodhaminiwa na Umoja wa Ulaya uliofanyika leo.