YAOUNDE: Kivuko chazima nje ya pwani ya Cameroon
6 Februari 2007Matangazo
Inahofiwa kuwa hadi watu 60 wamepoteza maisha yao baada ya kivuko kilichokuwa kikisafirisha abiria kati ya Cameroon na Nigeria kuzama nje ya pwani ya Tikioi,kusini-magharibi ya Cameroon.Maafisa wameanza kuchunguza sababu ya ajali hiyo.Mara kwa mara ajali hutokea kwenye pwani ya Cameroon kwa sababu ya vivuko kupakia abiria wengi kuliko inavyoruhusiwa na vivuko hivyo kukosa kufanyiwa ukarabati.