Mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo umebaki bila watu baada ya wakaazi kukimbia kufuatia onyo kuwa volkano ya Mlima Nyiragongo huenda ikaripuka tena. Mji huo umekuwa katika hali ya tahadhari baada ya kutokea mripuko wa volkano Jumamosi iliyopita na kusababisha vifo vya watu 32. Bruce Amani amezungumza na mwandishi wa DW huko Goma Benjamin Kasembe.