1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu saba wauawa kwa kuchomwa moto Malawi

Yusra Buwayhid2 Machi 2016

Polisi nchini Malawi wanasema genge moja la watu limewauwa watu saba kwa kuwachoma moto kwa madai ya kukutwa na mifupa ya binaadamu kwa ajili ya matumizi ya kichawi kusini mwa nchi hiyo.

https://p.dw.com/p/1I5aK
Unicef Foto des Jahren 2009 +++nur im Zusammenhang mit der Berichterstattung über die Preisverleihung UNICEF Foto des Jahres
Picha: Johan Bävman

Mkuu wa polisi wa wilaya ya Nsanje, Kirdy Kaunga, anasema watu hao walikutikana na mifupa ya binadaamu na genge hilo likajiamulia kuchukua hatua mikononi mwao kwa kuwawasha moto wakitumia petroli.

Maafisa wanasema bado wanaendelea na uchunguzi iwapo mifupa hiyo ilikuwa ni ya watu wenye ulemavu wa ngozi, yaani albino.

Katika nchi kadhaa za Kiafrika, zikiwamo Malawi, Msumbiji na Tanzania, watu wenye ulemavu wa ngozi huandamwa kwa mashambulizi yanayolenga kukatwa viungo vyao ambavyo hutumiwa kwenye mambo ya kishirikina.

Mwandishi: Yusra Buwayhid
Mhariri: Mohammed Khelef