1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu hamsini wauwawa kwenye ajali ya treni Pakistan

19 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CdUT

ISLAMABAD

Takriban watu hamsini wameuwawa wakati treni ilipoacha njia mapema leo hii kusini mwa Pakistan.

Ajali hiyo imetokea wakati mabebewa 14 kati ya mabehewa 16 ya treni hiyo ya abiria kutoka Karachi kwenda Lahore yalipoacha njia.

Polisi na watu wa kujitolea wanakimbilia eneo hilo lilioko kama kilomita 400 kusini mwa Karachi kuwaokowa wahanga ambapo inaripotiwa kwamba baadhi ya abiria wamenasa kwenye mabehewa ya treni.