1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 40 wauwawa katika ghasia kati ya Wahindu na Waislamu

Ibrahim Swaibu
5 Machi 2020

Maelfu ya waislamu nchini India wamekuwa wakiandamana kupinga kupitishwa kwa sheria ya uraia yenye utata inayojulikana kama 'CAA'

https://p.dw.com/p/3YuyE
Maelfu ya wandamanaji nchini India wakipinga sheria ya uraia 'CAA'
Maelfu ya wandamanaji nchini India wakipinga sheria ya uraia 'CAA'Picha: picture-alliance/AA/J. Sultan

Zaidi  watu 40 waliuliwa  katika makabiliano kati ya Wahindu na Waislamu nchini  India, wataalamu wa haki za binadamu wanasema huenda waislamu wakalazimika kutafuta makazi mapya katika maeneo yasio na idadi kubwa ya Wahindu kwa kuhofia kushambuliwa tena.

Makabiliano hayo kati ya waislamu na Wahindu ndio mabaya  zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini India katika miongo kadha iliopita, na yalizuka baada ya mandamano ya miezi kadha ya  kupinga  kupitishwa kwa sheria ya uraia yenye  utata.

Katika sheria hiyo, serikali ya India inataka kuwapa uraia wahamiaji wa dini ya Kihindu, Budha na wakristo  wanaokimbia unyanyansaji kutoka mataifa ya Pakistan Afghanistan na Bangladesh. Hatahivyo  sheria hiyo inayojulikana kama 'CAA' haiwajumuishi waislamu.

Tangu kupitishwa  ,mnamo Desemba mwaka jana, waislamu wamekuwa wakiandamana wakitaka sheria hiyo iondolewe. Pia wakiwa na hofu ya kuachwa nje bila uraia katika usajili wa orodha ya raia unaoatarajiwa kufanywa nchini humo.

Shiririka la Thomson Reuters limesema Alhamisi kuwa maelfu ya watu hasa waislamu wako katika hatari ya kulazimika kuyahama makazi yao kutokana na ghasia hizo ambapo Wahindu walionekana wakiwashambulia Waislamu katika mji mkuu New Delhi. Mtalaam wa haki za binadamu Miloon Kothari amesema kuwa baada ya ghasia hizo, serikali ya waziri mkuu Narendra Modi huenda  pia ikawatenga waislamu, kuwanyima huduma bora  pamoja na makazi mazuri. Ameliambia shirika la Thomsom Reuters.

Mapema Alhamisi polisi  walionekana wakipiga doria katika barabara za mtaa wa Shiv Vihar, Kaskazini mashariki mwa mji mkuu New Delhi ambapo mapambano  makali zaidi  yalitokea. 

Jamii ya Waislamu yaendelea kutengwa

Polisi wakikamata mwandamanaji wakati wa mandamano ya kumtaka waziri Amit Sha ajiuzulu
Wandamanaji pia wanamtaka waziri wa mambo ya ndani Amit Sha ajiuzuluPicha: Reuters/A. Fadnavis

Watalaamu wa haki za binadamu wanasema kuwa baada ya ghasia ziliowalenga waislamu katika mji wa  Mumbai mwaka 1992 na 1993 nchini humo, idadi kubwa ya waislamu walikimbilia  katika maeneo ya  jamii zenye waislamu peke kwa kuhofu kushambulliwa.

Darshani Mahadevia, profesa katika chuo kiku cha Ahmedabad ameeleza  kuwa  baada ya ghasia za mwaka 2002 katika Mji wa Ahmedabad, maelfu ya waislamu walilazimika kuhama kutoka miji idadi kubwa ya Wahindu na kwenda maeneo yasio miundombinu bora pamoja na kukosa makazi mazuri.

Mnamo Juma tatu wabunge nchini humo walipurukushiana bungeni baada ya vyama vya upinzani kumtaka waziri wa mambo ya ndani Amit Shah ajiuzulu kutokana na jinsi serikali ilivyojibu mandamano ya kupinga sheria hiyo na hata kusambabisha ghasia hizo.

Wabunge wa upinzani walionekana wakibeba mabango na kuimba kauli za kumtaka  waziri huyo ambaye pia ni mkuu wa polisi, ajiuzulu.

Chama tawala cha waziri mkuu Narendra Modi cha  Bharatiya Janata kimetetea sheria hiyo kikisema inalenga kulinda watu dini ndogo Kusini mwa bara la Asia lakini wanaharakati na wakosoajai wamesema sheria hiyo inawabagua waislamu na pia ni  kinyume na katiba  ya India ambayo haiendeshwi kwa msingi wa dini yoyote.

Vyanzo : AFPE/RTRE