1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanajeshi, waandamanaji Sudan waahidi kutekeleza makubaliano

Mohammed Khelef
8 Agosti 2019

Naibu Waziri wa Masuala ya Kisiasa wa Marekani, David Hale, amesema majenerali wa kijeshi na viongozi wa waandamanaji nchini Sudan wameahidi kuingia katika kipindi cha mpito kurejesha utawala wa kiraia.

https://p.dw.com/p/3NYcf
Sudan Abkommen - Ahmed Rabie und General Mohamed Hamdan Daglo
Picha: AFP/A. Shazly

Naibu waziri wa masuala ya kisiasa nchini Marekani David Hale, amesema jana kuwa majenerali wa kijeshi wanaoongoza nchini Sudan pamoja na viongozi wa waandamanaji wametoa ahadi thabiti za kuingia katika kipindi cha mpito kurejesha mamlaka kwa uongozi wa kiraia.

Hale amesema hayo baada ya kukutana na kiongozi wa baraza la kijeshi; Abdel Fattah al- Burhan, viongozi wa waandamanji na maafisa wa vyama vya kijamii.

Baraza la kijeshi linaloongoza na viongozi wa vuguvugu la maandamano nchini humo walitia saini maazimio siku ya Jumapili yanayotoa njia ya kurejeshwa kwa mamlaka kwa uongozi wa kiraia baada ya zaidi ya miezi saba ya maandamano na ghasia.

Akiwahutubia wanahabari wakati wa mkutano  mjini Khartoum, alipongeza mkataba huo, ulioongozwa na Ethiopia na Muungano wa Afrika na kuutaja kuwa wakihistoria.