1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanafunzi wa vyuo vikuu DRC waandamana

27 Aprili 2011

Polisi nchini Jamhuri ya Kidmokrasia ya Kongo wanapiga doria kwenye Chuo Kikuu cha Kinshasa kuwazuia wanafunzi wanaopinga kupandishwa kwa ada ya mtihani kutoka dola 5 za Kimarekani hadi 15.

https://p.dw.com/p/114t4
Wanafunzi wa "Institut National de Preparation Professionnelle" nchini DRC
Wanafunzi wa "Institut National de Preparation Professionnelle" nchini DRCPicha: AP

Vurugu za wanafunzi zimesababisha uharibifu chuoni hapo, ukiwemo kuvunjwa kwa vyoo vya ofisi ya chuo na magari ya walimu. Kwa mujibu wa watu walioshuhudia, mtu mmoja ameuawa, lakini Polisi wamekanusha, wakisema watu wamejeruhiwa tu, kama inavyosema ripoti ya Saleh Mwanamilongo aliyeko Kinshasa

Ripoti: Salehe Mwanamilongo
Mwandishi: Aboubakary Liongo
Mhariri: Othman Miraji