1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanadiplomasia wawili wapigwa marufuku kuingia Afghanistan.

26 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CgHy

Kabul.

Afghanistan imewaamuru wanadiplomasia wa Uingereza na Ireland kuondoka nchini humo. Maafisa wa serikali mjini Kabul wamesema kuwa watu hao wameamriwa kutoingia tena nchini humo baada ya madai kuwa walikutana na wapiganaji wa taliban wakati wa ziara yao katika jimbo la kusini lenye mapigano la Helmand. Mmoja kati ya watu hao waliotakiwa kuondoka nchini humo alikuwa mfanyakazi wa umoja wa mataifa na mwingine ni mfanyakazi wa umoja wa Ulaya.