Wabunge Tanzania wahofia maisha yao
25 Novemba 2014Hali kwenye mji mkuu wa Tanzania, Dodoma, ambako ndiko vinakoendelea sasa vikao vya bunge hilo inatajwa kuwa tete, chini ya masaa 24 kabla ya kuwasilishwa ripoti ya uchunguzi juu ya kashfa hiyo inayotajwa kuwa moja ya kashfa kubwa kabisa kuwahi kulikumba taifa hilo la Afrika ya Mashariki ikiwahusisha vigogo na wafanyabiashara kadhaa.
Mohammed Khelef alizungumza na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, ambaye ndiye kwa mara ya kwanza aliyeiibua kashfa hiyo bungeni na ambaye, pamoja na wabunge wengine kadhaa wanaopigania kuwajibishwa kwa wahusika, analalamikia kutishiwa usalama wa maisha yao.
Kusikiliza mahojiano kamili, tafadhali bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Mwandishi: Mohammed Khelef
Mhariri: Mohamed Abdul-Rahman