Mjadala kuhusu mishahara na marupurupu ya wabunge nchini Kenya bado unaendelea na wanaharakati wanashikilia kuwa wabunge warudishe fedha walizolipwa kimakosa. Je kuna uwezekano upi wa fedha hizo kurudishwa? Kuhusu hilo, DW imezungumza na mwanaharakati wa kisiasa nchini Kenya aliyeko Nairobi Gachihi Gacheke na kwanza anaelezea kero ya wakenya dhidi ya tamaa ya wabunge nchini humo.