1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Ulaya wakutana na wenzao wa Afrika Abidjan

Oumilkheir Hamidou
29 Novemba 2017

Viongozi wa Umoja wa ulaya wameanza mazungumzo yao pamoja na viongozi wenzao wa bara la Afrika kuhusu uhamaji, wakipania kuupatia ufumbuzi mzozo wa watu wanaoyatia hatarini maisha yao kwa lengo la kuingia barani Ulaya.

https://p.dw.com/p/2oUPb
EU-Afrika-Gipfel in Abidjan
Picha: picture-alliance/dpa/M. Kappeler

Viongozi kutoka Ufaransa, Ubeigiji, Luxemburg, wote wakiwa ni viongozi wa kiume wenye umri unaokurubia miaka 40 wanajaribu kujitenganisha na picha ya wakoloni wa zamani wa Afrika, wakitetea umuhimu wa kuendeleza biashara na kuwekeza katika miradi ya maendeleo na usalama barani humo pamoja na kushughulikia vyanzo vya uhamaji.

Uhamaji ndio mada kuu katika mkutano huu wa kilele mjini Abidjan, mji mkuu wa kibiashara wa Côte d'Ivoire, mada iliyopata nguvu kutokana na kanda ya video iliyotangazwa hivi karibuni na kituo cha televisheni cha CNN  na kuonyesha jinsi vijana wa kiafrika walivyokuwa wakiuzwa kama watumwa katika masoko ya mnada nchini Libya. Akizungumza kuhusu kisa hicho cha karaha, kansela Angela Merkel amesema:"Mada ya uhamaji kinyume na sheria inakamata nafasi muhimu katika bara lote la Afrika wakati huu tulio nao kwasabau kuna rirpoti zinazosema vijana wa kiafrika wamekuwa wakiuzwa kama watumwa nchini Libya. Na hiyo ndio sababu mada hiyo inazusha jazba kubwa katika mkutano huu. Kwa hivyo yameibuka masilahi ya pamoja ya kukomesha uhamaji kinyume na sheria na kuwafungulia njia watu kutoka Afrika kuweza kuja Ulaya kusoma au kujifunza kazi."

Kansela Angela Merkel akizungumza na mwenyeji wakle, rais Alassane Ouattara wa Côte d'Ivoire
Kansela Angela Merkel akizungumza na mwenyeji wakle, rais Alassane Ouattara wa Côte d'IvoirePicha: picture-alliance/dpa/M. Kappeler

Biashara ya watumwa ni uhalifu dhidi ya ubinaadam

Kansela Merkel amesema hayo mwanzoni mwa mkutano wa kilele wa viongozi wa Umoja wa ulaya na Afrika mjini Abidjan. Jana usiku rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aliitaja biashara ya wahamiaji wa kiafrika kuwa "uhalifu dhidi ya ubinaadam. Macron amesema anataka nchi za Ulaya na zile za Afrika ziwasaidie watu waliokamwa nchini Libya ili waweze kurejeshwa makwao. Aliahidi kufafanua zaidi kuhusu juhudi hizo katika mkutano huu wa kilele ulioanza hivi punde mjini Abidjan.

Meli ya kuwaokoa wakimbizi wa Afrika wanaoelekea Ulaya kupitia bahari ya kati
Meli ya kuwaokoa wakimbizi wa Afrika wanaoelekea Ulaya kupitia bahari ya katiPicha: picture-alliance/dpa/L. Klimkeit

 Viongozi vijana wa Ulaya wanataka kuondokana na sura ya wakoloni wa zamani

Waziri mkuu wa ubeligiji, Charles Michel amewahimiza viongozi wenzake wa Ulaya washirikiane kwa dhati zaidi na wenzao wa Afrika katika suala la uhamaji na usalama, mada ya pili muhimu itakayojadiliwa katika mkutano huu wa kilele wa siku mbili mjini Abidjan.

Tunachokitaka ni mkakati utakaoleta manufaa kwa pande zote mbili amesema Michel mwenye umri wa miaka 41. Ameongeza kusema anatoka katika kizazi kinacholiangalia bara la Afrika kama mshirika, hakuna upenu katika kizazi chetu wa kufikiria yaliyotokea zamani" amesema waziri mkuu huyo wa Ubeligiji aliyefuatana na mwenzake wa Luxemburg Xavier Bettel, wakionyesha sura tofauti na ile ya walio watangulia.

 

Mwandishi:Hamidou Oummilkheir/AP

Mhariri: Josephat Charo