1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa Sudan na Sudan kusini wakutana Addis

5 Januari 2013

Viongozi wa Sudan na Sudan kusini wamekutana Ijumaa(04.01.2013)kuondoa hali ya wasi wasi ambayo imetanda tangu kusini kujitenga mwaka 2011 na kuanza usafirishaji mafuta ili kukwamua uchumi wa nchi hizo unaodidimia.

https://p.dw.com/p/17ERx
(L-R) Pagan Amum, south Sudan chief negotiator, South Sudan's President Salva Kiir, former president of Nigeria Abdulsalam Abubakar, Chief African Union mediator Thabo Mbeki, former Burundi president Pierre Buyoya and President of Sudan Omar Hassan al-Bashir meet during talks in Ethiopia's capital Addis Ababa September 24, 2012. Leaders from Sudan and South Sudan will meet on Sunday for the first time in a year to try to agree on border security so that South Sudan can start exporting oil again, a lifeline for both economies. REUTERS/Tiksa Negeri (ETHIOPIA - Tags: BUSINESS COMMODITIES POLITICS)
Mkutano uliopita kati ya Sudan na Sudan kusini mjini Addis AbabaPicha: Reuters

Hakuna taarifa zaidi zilizojitokeza wakati rais wa Sudan Omar al-Bashir na Salva Kiir wa Sudan ya kusini walipokutana pamoja na waziri mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn, ambaye anajaribu kufanya upatanishi kati ya nchi hizo jirani ambazo zilikaribia kupigana vita mwezi wa Aprili.

Sudan's President Omar Hassan al-Bashir (L) meets his host, the new Ethiopian Prime Minister Hailemariam Desalegn, at the Palace in capital Addis Ababa September 23, 2012. Leaders from Sudan and South Sudan will meet on Sunday for the first time in a year to try to agree on border security so that South Sudan can start exporting oil again, a lifeline for both economies. REUTERS/Tiksa Negeri (ETHIOPIA - Tags: POLITICS BUSINESS CIVIL UNREST)
Rais Omar al-Bashir akikutana na waziri mkuu wa Ethiopia Hailemariam DesalegnPicha: Reuters

Viongozi wote hao wawili watakutana kwa mara ya kwanza peke yao katika mkutano utakaofanyika hii leo Jumamosi (05.01.2013), limeeleza shirika la habari la Sudan SUNA.

Makubaliano hayakutekelezwa

Sudan na Sudan kusini tayari zimekubaliana mwezi Septemba kuanza tena kwa mauzo ya mafuta na kuhakikisha usalama wa mpaka wao ambao mara kwa mara huzuka mapigano , lakini zilishindwa kufuatilia utekelezaji kutokana na kuwapo hali ya kutoaminiana, hali inayokutikana katika mataifa hayo ya Afrika ambayo yamepigana vita virefu vya wenyewe kwa wenyewe.

BRUSSELS, March 20, 2012 President of South Sudan Salva Kiir Mayardit speaks during a press briefing after meeting with President of European Commission Jose Manuel Barroso (not seen) at the EU headquarters in Brussels, capital of Belgium, March 20, 2012
Rais wa Sudan kusini Salva Kiir MayarditPicha: picture alliance / ZUMA Press

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema mvutano huo umesaidia kuongeza umaarufu ndani ya nchi hizo kwa serikali zote kwa kuondoa mtazamo kutoka katika matatizo yao ya kiuchumi na kutapakaa kwa rushwa.

Lakini uchumi wa nchi hizo mbili jirani unategemea sana mapato yatokanayo na nishati na zinahitaji mafuta kusafirishwa kutoka katika visima katika Sudan ya kusini.

Serikali ya kusini mjini Juba ilifunga visima vyake vyote vinavyotoa kiasi ya mapipa 350,000 mwaka mmoja uliopita baada ya kushindwa kukubaliana juu ya kodi ya mauzo ya nje.

Upande wa kaskazini unaitoza Sudan kusini mamilioni ya dola kwa mwezi kwa kupitisha mafuta ghafi katika ardhi yake na kuyauza nje kupitia kituo kilichoko katika bahari ya Sham.

Chini ya makubaliano yaliyofikiwa mwezi Septemba , wamekubaliana kuyaondoa majeshi yao kutoka katika mpaka ambao una umbali wa kilometa 2,000, eneo ambalo kwa kiasi kikubwa linagombaniwa na nchi hizo.Pande zote mbili zinasema eneo kama hilo lisilokuwa na shughuli za kijeshi ni muhimu kabla ya mafuta kutoka Sudan kusini ambayo haina bandari yataweza kutiririka tena kupitia ardhi ya Sudan.

epa02521154 A Southern Sudanese man holds a Southern Sudan flag during the referendum on the independence of South Sudan at a polling station in Juba, Southern Sudan, 09 January 2011. Southern Sudanese went to the polls in a historic referendum that is widely expected to see them vote to split from the north. The week-long vote is the centerpiece of a 2005 peace deal that ended decades of civil war between the mainly Muslim north and the Christian and Animist south - a conflict which claimed the lives of more than 2 million southerners and displaced 4 million more. An emotional Salva Kiir, president of Southern Sudan, choked back tears as he cast his ballot and dedicated the vote to independence leader John Garang - who died in a 2005 helicopter crash - and all those who perished in the war. Just under 4 million Southern Sudanese are registered to put a thumbprint on the ballot - either under a picture of two hands clasping for unity, or one held up as if waving goodbye for secession. Few doubt that jubilant and expectant Southern Sudanese will vote for independence, but at least 60 per cent of registered voters must turn out for the referendum to be valid. The vote, which many had doubted would take place on time, has raised fears of a return to conflict between north and south. EPA/MOHAMED MESSARA +++(c) dpa - Bildfunk+++ usage Germany only, Verwendung nur in Deutschland
Bendera ya Sudan Kusini baada ya uhuruPicha: picture-alliance/dpa

Lawama kila upande

Jana Ijumaa(04.01.2013), kiongozi wa ujumbe wa Sudan ya kusini katika majadiliano hayo Pagan Amum ameishutumu Sudan kwa kudondosha mabomu katika eneo la mpaka mara nne wiki hii. Jeshi la Sudan halikupatikana mara moja kutoa maelezo yake lakini kila mara inakana madai hayo.

"Hii kwa kweli ni hali ambayo si nzuri. Mashambulizi haya ya anga yanaleta athari ambayo si nzuri katika mkutano na majadiliano," Amum amewaambia waandishi habari mjini Addis Ababa.

Kwa upande wake Sudan nayo inailaumu mara kwa mara Sudan ya kusini kwa kuwaunga mkono waasi wa Sudan People's Liberation Movement- North (SPLM-North) katika majimbo mawili ya mpakani. Serikali ya Sudan kusini inakana shutuma hizo na kusema Sudan inawaunga mkono wanamgambo katika ardhi yake.

A soldier of South Sudan's SPLA army holds his rifle near an oil field in Unity State April 22, 2012. REUTERS/Goran Tomasevic (SOUTH SUDAN - Tags: MILITARY CIVIL UNREST) Die Sudanesische Volksbefreiungsbewegung (englisch Sudan People’s Liberation Movement, abgekürzt SPLM; arabisch ‏الحركة الشعبية لتحرير السودان‎) ist eine politische Partei und ehemalige Widerstandsbewegung im Sudan und im Südsudan.
Wapiganaji wa SPLM-kaskaziniPicha: Reuters

Wanadiplomasia wanasema kuwa pande zote mbili zinaichukulia mikutano kama hiyo kuwa ni nafasi ya kugusa maeneo dhaifu ya upande mwingine badala ya kuwa ni fursa ya kutatua matatizo yao.

Wakati huo huo maafisa wa Sudan kusini wamesema kuwa rais wa nchi hiyo anatarajiwa kupendekeza matumizi ya upatanishi wa lazima wa kimataifa ili kutatua mzozo wa mpaka na Sudan.

Mwandishi: Sekione Kitojo / ape/ rtre / dpae

Mhariri : Abdu Mtullya