Huku Sekta ya teknologia ikiendelea kustawi barani Afrika na maendeleo yake yakizidi kupanuka, idadi ya wanawake kwenye taaluma hiyo ingali inatajwa kuwa ndogo ikilinganishwa na wanaume. Mjini Mombasa kuna mradi wa teknolojia ulioanzishwa na kundi la wasichana kupitia shirika lao linalojulikana kama "Pwani Techknowgalz" kuwahamasisha watoto wa kike kuhusiana na maswala ya teknolojia.