Shirika la kuwahudumia Watoto la Umoja wa Mataifa, Unicef limesema katika ripoti yake mpya, kwamba idadi ya wasichana wanaoolewa wakiwa bado watoto imepungua kwa kiwango kikubwa duniani. Ingawa limeonya kwamba hadi kufikia 2030, wasichana wapatao milioni 150 wanakabiliwa na hatari ya kuozwa kabla ya kutimiza miaka 18. Papo kwa Papo 06.03.2018