1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujumbe wa Noel kutoka rais wa Ujerumani-vijana na wazee mheshimiane

24 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/Cfjx

BERLIN:

Rais wa Ujerumani,Horst Köhler ametoa mwito kuwepo ushirikiano zaidi kati ya wazee na vijana wa hapa Ujerumani akisema pande zote mbili zinaweza kufaidika na hatua hiyo.Katika ujumbe wake wa Krismas, Bw Köhler amesema kuwa vitu vizuri hutokea maishani wakati wa ujana. Pia amewashukuru wanajeshi wa nchi hii ambao wakati huu wa sikukuu wako kazini nje ya nchi.