Mbunge wa upinzani Uganda Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine aliachiwa huru kwa muda na mahakama ya kijeshi Uganda baada ya serikali kuyafuta mashitaka yote yanayomkabili kwa kuonesha hali ya kutokuwa na haja ya kuendelea na kesi hiyo. Lakini muda mfupi baadae alitiwa tena mbaroni. Sikiliza mahojiano kati ya Sudi Mnette na mwandishi habari Kassim Kayira, akiwa Kampala. Je Bobi anaweza kuwa huru?