Siku moja ukiwa umeketi mgahawani, jaribu kufuatilia meza iliyo na kundi la watu wengi hasa vijana, kisha subiri chakula chao kinapoletwa mezani. Kwa haraka sana, simu zao zinaanza kufanya kazi moja ya kupiga picha za vyakula vilivyo mezani. Kutokana na hali hiyo baadhi ya migahawa duniani imeanza kuwa na ubunifu unaovutia watumiaji wa mitandao kama Instagram. Ungana naye Sylvia Mwehozi.