1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump awasili Davos

Sekione Kitojo
25 Januari 2018

Akishikilia silaha yake ya nadharia ya "Amerika kwanza" rais Donald Trump aliwasili Uswisi kutetea ajenda yake hiyo ya kiuchumi katika  kongamano la kiuchumi ambalo linasisitiza biashara na ushirikiano wa kimataifa.

https://p.dw.com/p/2rW6I
Schweiz Ankunft Trump in Zürich
Picha: Getty Images/AFP/N. Kamm

Trump  aliwasili  mjini  Zurich kabla  ya  muda  uliopangwa  na  mara moja  alipanda  katika  helikopta  ya  Marekani  kwa  ajili  ya  safari kwenda  Davos, ambako  kongamano la  kiuchumi  duniani linafanyika. Safari  hiyo  ya  takriban dakika  40 ilimchukua  Trump akipita  katika  mandhari  ya  nchi  iliyofunikwa  na  barafu , hapa  na pale  kukiwa  na  nyumba , milima  iliyovunikwa  na  theluji  pamoja na  ziwa zililoganda  barafu.

Schweiz, World Economic Forum in Davos
Eneo la Davos lililofunikwa na barafu Picha: picture-alliance/D.Keyton

Wakati  Trump  aliposhuka  kutoka  katika  helikopta  hiyo  mjini Davos, aliwaangalia  wasaidizi  wake  ambao  walimshika  mkono wakati  akitembea  katika  eneo  la  kutua  na  ambalo  limejaa theluji hadi  katika  gari  yake iliyokuwa  ikimsubiri.

Wakati  rais  Trump  anatarajiwa  kutangaza  kwamba  Marekani  iko wazi  kwa  ajili  ya   kufanya biashara , kuhudhuria  kwa  rais  huyo ambaye  anaelemea  kulinda  masoko  ya  nchi  yake  katika mkusabyiko  huko  wa  kila  mwaka  kwa  watu  mashuhuri , wanasiasa  na  wafanyabiashara  ambao  hupendelea  biashara huria , amewashitua  wengi.

Uamuzi  wake  wiki  hii  kutia  saini matumizi  ya kodi  mpya  inayoimarisha  viwanda  vya  Marekani imezusha  wasi  wasi  mpya  juu  ya  mwelekeo  wake  wa  siasa  za kizalendo  zaidi.

USA Donald Trump
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: picture-alliance/AP Photo/C. Kaster

Trump atamba

"Ninakwenda  Davos  hivi  sasa  kuwezesha  watu  kuwekeza  nchini Marekani," Trump  alisema  jana  kabla  ya  kupanda  ndege  kwenda barani  Ulaya. "Nitawaambia : njoni  Marekani. Mna  fedha  nyingi." Lakini  sifikiri  kama  ni  muhimu  kwenda, kwasababu  wanakuja, wanakuja kwa  haraka  sana."

Katika  maelezo  yake  katika  ukurasa  wa  Twitter aliyoandika kabla  kuondoka  Ikulu  ya  Marekani  ya  White House Trump alisema, "Uchumi  wetu unakua  kwa  kasi na  kwa  kila  kitu ninachofanya , utaendelea  vizuri  tu.. nchi  yetu  hatimaye inashinda tena!"

Waziri  mkuu  wa  Uingereza  Theresa  May  alipoulizwa  kuhusu iwapo  atazungumza  na  Trump  kuhusu biashara  huru , alisema.

"Biashara  huru  ni  mada  ambayo  niliijadili  na  rais hapo  zamani. Tuna  shauku  kubwa  kwamba  tutaweza kufanya  hivyo na Marekani wakati  tutakapoondoka  katika  Umoja  wa  Ulaya. Wanashauku  kubwa  kwa  hilo, na sisi  pia tunashauku na  tayari tunalifanyia  kazi juu  ya  vipi tutatekeleza  hilo".

Theresa May beim Weltwirtschaftsforum in Davos
Waziri mkuu wa Uingereza Theresa MayPicha: Reuters/D. Balibouse

Waziri  wa  fedha  wa  Marekani  Steven  Mnuchin  aliwasili  mjini Davos  kabla  ya  Trump  na  kusisitiza  kwamba  Marekani  inaunga mkono  biashara  huru.

Waziri  wa  biashara  wa  Marekani  Wilbur Ross amedai  kuwa kodi mpya  nchini  Marekani  kwa  vifaa  vinavyoagizwa  kutoka  nje  vya nishati  ya  jua , solar pamoja  na  mashine  kubwa  za  kufulia zina lenga  kupambana  na  tabia  ambazo  hazistahili za   baadhi  ya mataifa  na  sio kulinda  masoko. Pamoja  na  hayo  Ross  alikiri kwamba  China  inaweza  kujibu  hali  hiyo  kwa  kuweka kodi  zake kwa  biadhaa  za  Marekani.

Mwandishi: Sekione  Kitojo ape /afpe

Mhariri: Iddi Ssessanga