Tottenham yamtimua kocha Andre Villas Boas
16 Desemba 2013Klabu hiyo imesema katika taarifa kuwa uamuzi huo umetokana na “makubaliano na maslahi ya pande zote mbili”. Kichapo dhidi ya Liverpool kimewaweka katika nafasi ya saba kwenye Premier League, point I nane nyuma ya viongozi Arsenal na tano nyuma ya nafasi ya kucheza katika Champions League.
Villas Boas alichukua uongozi mwanzoni mwa msimu, na amekuwa chini ya mbinyo kutoka mwanzo baada ya kutumia kiasi cha zaidi ya pauni milioni 100 kwa kuwasajili wachezaji wapya, ijapokuwa alipata pauni milioni 85 kutoka kwa mauzo ya Gareth Bale aliyehamia Real Madrid. Jana usiku Villas Boas aliahidi kuwa hawezi kung'atuka akisema wachezaji wake watajinyanyua tena haraka na kuendelea kupigania nafasi nzuri.
Mwandishi: Bruce Amani/DPA/AFP
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman