1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TEL AVIV:Olmert ndani ya mbinyo mkubwa

4 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CC4w

Inakadiriwa kiasi cha watu laki moja wameandamana hapo jana katika mji mkuu wa Israel Tel Aviv kumshinikiza Waziri Mkuu wa nchi hiyo Ehud Olmert ajiuzulu.

Maandamano hayo yamekuja saa chache tu baada ya bunge kuanza mjadala juu ya hatima ya bwana Olmert kuendelea kuwa Waziri Mkuu wa Israel.

Pamoja na kutolewa kwa wito wa kujiuzulu kutoka upande wa upinzani, hakuna kura yoyote ya kutokuwa na imani naye iliyopigwa.

Hali hiyo iliongezwa utambi siku ya jumatatu baada ya kutolewa ripoti, iliyoelezea jinsi serikali ya Olmert ilivyoshughulikia vita vya nchi hiyo na wanamgambo wa Hezbollah nchini Lebanon.

Hapo siku ya Jumatano, Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Tzipi Livni ambaye anatoka katika chama cha Bwana Olmert alimtaka Waziri Mkuu huyo ajiuzulu.