1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Takaichi, Trump kuangamiza zana za nyuklia Korea Kaskazini

28 Oktoba 2025

Waziri Mkuu wa Japan Sanae Takaichi, amesema yeye pamoja na Rais wa Marekani Donald Trump wamethibitisha kwa mara nyengine dhamira yao ya kukamilisha uangamizaji wa silaha za nyuklia za Korea Kaskazini.

https://p.dw.com/p/52h4Z
Japan Yokosuka 2025 | Donald Trump und Sanae Takaichi besuchen US-Flugzeugträger USS George Washington
Picha: Andrew Caballero-Reynolds/AFP

Takaichi amesema viongozi hao wawili wamekubaliana hayo katika mkutano wa kilele leo huko mjini Tokyo.

Takaichi na Trump vile vile wamesisitiza umuhimu wa amani Taiwan ingawa amekataa kutoa tamko lolote juu ya walichokijadili kuhusu China kwa sababu Trump atakutana na Rais wa China hivi karibuni.

Haya yanafanyika wakati ambapo mtu mmoja anayetuhumiwa kumuua kwa kumpiga risasi waziri mkuu wa zamani wa Japan Shinzo Abe miaka mitatu iliyopita, leo amekiri kumuua kiongozi huyo, wakati kesi dhidi yake ilipokuwa ikisikilizwa kwa mara ya kwanza.

Tetsuya Yamagami mwenye umri wa miaka 45 alikamatwa katika eneo la tukio hilo Julai 2022 baada ya kudaiwa kumfyetulia risasi Abe aliyekuwa anahutubia umati wa watu wakati wa kampeni za uchaguzi katika mji wa magharibi wa Japan wa Nara.