Nchini Kenya, katika kijiji kimoja kilichopo karibu na mpaka na Somalia, kaunti wa Wajir, kumezuka taharuki baada ya kuokotwa kichwa cha naibu kiongozi pasipo kiwiliwili chake. Bwana huyo Omar Aden Buul alitekwa nyara Ijumaa iliyopita na kundi la wanamgambo la Al-Shaabab. DW imezungumza na Kamanda wa Polisi wa Jimbo la Wajir, Hillary Rwaichichi, kwanza anaelezea hali ya usalama kwa sasa.