1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMali

Mali: Shule zafungwa kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta

27 Oktoba 2025

Mamlaka za Mali zimechukua hatua ya kufunga shule na vyuo vikuu kwa muda wa wiki mbili kufuatia uhaba mkubwa wa mafuta.

https://p.dw.com/p/52eU1
Bamako | Uhaba mkubwa wa mafuta umeshuhudiwa kote nchini Mali
Mali imechukua hatua ya kufunga shule kutokana na uhaba mkubwa wa mafutaPicha: Idriss Sangare/REUTERS

Uhaba huo umesababishwa na vizuizi vilivyowekwa na wanamgambo wenye mafungamano na kundi la kigaidi la Al-Qaeda. Mapema mwezi Septemba, wanamgambo wa  Jama'at Nusrat al-Islam wal-Muslimin (JNIM)  walitangaza kuzuia uagizaji wa mafuta katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi isiyo na bandari, na tangu wakati huo wamekuwa wakishambulia misafara ya malori ya mafuta yanayojaribu kuingia nchini humo.

Hatua hii inatajwa na wachambuzi kuwa ni sehemu ya kampeni ya makundi hayo ya wanamgambo na inayolenga kuzidisha shinikizo kwa serikali ya kijeshi ya  Mali kwa kuzuia chanzo kikuu cha uchumi nchini humo.