1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shirika la UNICEF nchini Kongo limeingilia kati kuhusu kuachiwa kwa watoto 80 walioshikiliwa na waasi wa LRA

24 Septemba 2008

Juhudi za serikali ya DRC ya kuwasaka waasi wa FDRL wa Rwanda na wale wa LRA wa Uganda zikingali mbali kuzaa matunda mazuri kwa raia wa kongo.

https://p.dw.com/p/FO4U
Waasi wa LRAPicha: AP Photo

Wiki iliopita watoto zaidi ya 80 wa shule ya msingi walikamatwa na kupelekwa porini na waasi wa LRA baada ya kuunguza shule yao kwenye mji wa DUNGU jimboni ORIENTALE.Shirika la UNICEF limeomba kuachiliwa kwa watoto hao,kama anavyoripoti mwandishi wetu Saleh Mwanamilongo.