1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Schalke yaendelea kumwinda Sami Khedira

2 Mei 2015

Kiungo wa Ujerumani Sami Khedira anasalia kuwa mchezaji anayemulikwa sana wakati klabu ya Schalke ikijiandaa kufanya mabadiliko katika kikosi chacke kwa ajili ya msimu ujao.

https://p.dw.com/p/1FJ64
Bildergalerie Berühmte Männer in Europa mit arabischem Hintergrund
Picha: picture-alliance/dpa/Marcelo Sayao

Mwenyekiti wa bodi ya klabu hiyo ya Bundesliga Clemens Toennis amesema “kutakuwa na mabadiliko” wakati Schalke ikiwa na msimu ambao haijaweza kufuzu katika nafasi ya kucheza Ligi ya mabingwa msimu ujao.

Toennies hajatoa maelezo zaidi lakini amesisitiza kuwa Schalke inamtaka Khedira mwishoni mwa msimu huu wakati mkataba wake katika klabu ya Real Madrid utakapofikia kikomo, mradi tu makubaliano mazuri ya kifedha yatafikiwa na mchezaji huyo. Schalke iko katika nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi wakati kukisalia na mechi nne msimu kukamilika.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/AP/DPA/Reuters
Mhariri: Mohamed Daman