SiasaSerbia
Rais wa Serbia aachia uongozi wa chama tawala
27 Mei 2023Matangazo
Kwenye kongamano la chama hicho, Vucic amemteua waziri wa ulinzi Milos Vucecic kuchukua nafasi hiyo, ingawa mchakato mzima unatakiwa kuidhinishwa rasmi katika kikao cha ndani cha chama hicho.
Vyama vya upinzani na wanaharakati wa haki za binaadamu kwa muda mrefu wamemtuhumu Vucic na chama chake kwa utawala wa kibabe, kuviminya vyombo vya habari, kuwaonea wapinzani, ufisadi na kujihusisha na uhalifu wa kupangwa.
Hatua hii inachukuliwa siku moja baada ya maelfu ya raia kuandamana kote nchini Serbia na mataifa jirani ya Kosovo, Montenegro na Bosnia, ya kumuunga mkono rais Vucic baada ya maandamano makubwa ya kumpinga.
Soma Zaidi: Serbia yaagiza wanajeshi kuukaribia mpaka na Kosovo baada ya makabiliano ya waandamanaji