1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Italia aitisha kikao na viongozi wa vyama

Sekione Kitojo
3 Mei 2018

Rais wa Italia Sergio Mattarella ameitisha duru mpya ya mashauriano na viongozi wa vyama hapo Mei 7 kujaribu kumaliza wiki tisa za  misuguano mikali ya mkwamo wa kisiasa kufuatia uchaguzi ambao haukuweza kumpata mshindi.

https://p.dw.com/p/2x822
Italien Präsident Sergio Mattarella löst Parlament auf
Picha: Reuters/Presidential Press Office

Mattarella  tayari  amefanya  vikao  viwili  vya  mazungumzo ambavyo  vimeshindwa  kufikisha  mwisho  mkwamo  wakati  juhudi mbili  zaidi  za  upatanishi zilizofanywa  na  spika  wa  bunge  pia ziligonga  mwamba.

Italien Gespräche über Regierungsbildung ergebnislos vertagt | Luigi Di Maio
Viongozi wa chama cha Nyota 5 , 5 StarPicha: Getty Images/AFP/A. Pizzoli

"Baada  ya  miezi  miwili, msimamo  wa  awali  wa  vyama umebadilika. Hakuna matumaini  yalijitokeza  kupata  serikali, ofisi ya  mkuu  wa  taifa  hilo  imesema, na  kuongeza  kwamba  rais alitaka  kusikia  iwapo viongozi  wa  chama  wana  mawazo mengine.

Nafasi  za  Mattarella  zinapungua  kwa  kasi  sana  na  uwezekano wa  kurejea  katika  uchaguzi  wakati  fulani  kati  ya sehemu  ya mwisho  ya  mwaka  huu  na  miezi  ya  mwanzo  ya  mwaka  ujao inaonekana  kuzidi  kupanda.

Uchaguzi  wa  taifa  Machi  4 ulishuhudia  muungano  wa  siasa  za wastani  za  mrengo  wa  kulia  ukiongozwa  na  chama  kinachopinga wahamiaji  cha  League  ukishinda  viti  vingi  na  kile  kinachopinga utawala  cha  5Star kikitokeza  kuwa  chama  kikuu. Chama  cha siasa  za wastani  za  mrengo  wa  kushoto  cha  Democratic PD kilishika  nafasi  ya  tatu.

Hatua  kadhaa  za  kutumia  kura  ya  turufu  zimezuwia  hadi  sasa vyama  hivyo  kukubaliana  juu  ya  muungano, huku misuguano  na kukata  tamaa  kukiongezeka siku  baada  ya  siku.

Italien Gespräche über Regierungsbildung ergebnislos vertagt | Matteo Salvini
Matteo Salvini kiongozi wa chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha LigaPicha: Getty Images/AFP/T. Fabi

Uchaguzi mpya

Kusisitiza  hali ya  hisia  ya  kupooza, chama  cha  PD  kilikuwa kiamue  baadaye  leo Alhamis  iwapo  kufungua  mazungumzo  rasmi na  chama  cha 5Star. Hata  hivyo, Mattarella  hakutaka  kusubiri uamuzi  wao  kabla  ya  kutangaza  mkutano  huo siku  ya  Jumatatu, ikiwa  ni  kukiri  kwamba  chama  hicho  kilichogawika  mno hakitaweza  kukubaliana  kuhusiana  na  suala  hilo.

Baada  ya  kufikia  uamuzi  kama  huo, kiongozi  wa  Nyota 5 wiki  hii alitoa  wito  wa  kufanyika  uchaguzi  mpya  mwezi  Juni, lakini  duru katika  ofisi  ya  rais  imeliambia  shirika  la  habari  la  Reuters jana kuwa  kiongozi  wa  nchi  atakataa  madai  hayo.

Badala  yake, Mattarella  anataka  kuunda  serikali  ya  muda  ili kutayarisha  bajeti  ya  mwaka  2019  ambayo  itaidhinishwa  ifikapo mwishoni  mwa  mwezi  Desemba.

Iwapo  viongozi  wa  vyama  watashindwa  kukubaliana  na  utawala wa  aina  hiyo , ambao bila  shaka  utaongozwa  na  mtu  ambaye  si mwanasiasa, kwa  hiyo  uchaguzi  ujao  utafanyika  mwishoni  mwa mwaka  huu , ama  huenda  mwezi  Oktoba.

Mawaziri  wakuu  wa  mwisho  wa  Italia  waliingia  madarakani kutokana  na  makubaliano  ya  nyuma  ya  pazia  badala  ya  ushindi katika   masanduku  ya  kura  na  juhudi  za  mara  kwa  mara kufanyia  mageuzi  sheria  za  uchaguzi  ambazo  zitaruhusu kuundwa  haraka  kwa  serikali  zimeshindwa  kuleta  mfumo  wa ushindi.

Italien Gespräche über Regierungsbildung ergebnislos vertagt | Giorgia Meloni
Kiongozi wa chama cha mrengo wa kulia cha Fratelli d'Italia , Georgia Meloni Picha: Getty Images/AFP/F. Frustaci

Mfumo mpya wa  uchaguzi

Wakati  chama  cha  Nyota 5 kinataka  kurejewa  kwa  uchaguzi haraka , vyama  vingine  vimeshauri  kufanyakazi  kwa  pamoja kutengeneza  mfumo  mpya  wa  uchaguzi. Hata  hivyo , kupata kuungwa  mkono  kwa  makubaliano  kama  hayo   katika  hali  ya sasa  ya  kisiasa  kunaonekana  hakuwezekani.

Wakati uongozi  wa  siku  hadi  siku  nchini  Italia unafanywa  na waziri  mkuu  mlezi  Paulo Gentiloni , matarajio ya  hivi sasa  ya kiuchumi  kutoka  katika  halmashauri  ya  Ulaya yamesisitiza  haja ya  kuwapo  na  serikali  kamili  ambayo  itakuwa  tayari  kufanya mageuzi.

Utabiri  unaonesha  kwamba  uchumi  wa  Italia  unatarajiwa  kukua kwa  asilimia  1.5  mwaka  huu  na  kiasi  ya  asilimia  1.2 tu mwaka ujao ikiwa  ni  kiwango  cha  chini  kabisa  miongoni  mwa  mataifa 27  wanachama  wa  Umoja  wa  Ulaya.

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre

Mhariri: Mohammed  Abdul-Rahman