1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Putin ahimiza ushirikiano na Afrika

Sekione Kitojo
23 Oktoba 2019

Rais Vladimir Putin amesema Urusi italenga kuongeza biashara na mataifa ya Afrika maradufu katika muda  wa miaka mitano ijayo, wakati  akifungua mkutano wa kilele wenye lengo la kufufua mahusiano ya Moscow na bara hilo.

https://p.dw.com/p/3RmzE
Sotschi Russland-Afrika Gipfel Ägypten
Picha: picture-alliance/dpa/S. Fadeichev

Rais  wa  Urusi amekuwa  mwenyeji  wa  viongozi  kadhaa  wa mataifa  ya  Afrika  leo kwa  mkutano  wa  kwanza  wa  kilele  kati  ya Urusi  na  bara  la  Afrika, na  kuakisi msukumo  mpya  wa  Urusi kupanua  ushawishi  wake  katika  bara  hilo na  kusema  kuna nafasi  kubwa  sana  kwa  ukuaji wa  uhusiano  huo.

Der russische und der ägyptische Präsident bei Ihrem Gipfeltreffen in Sotschi
Wenyeji wa mkutano kati ya Urusi na Afrika , marais Vladimir Putin wa Urusi (Kushoto) na Abdel Fattah el-Sissi wa Misri mjini Sochi.Picha: picture-alliance/dpa/V. Sharifulin

Putin na  rais  wa  Misri Abdel-Fattah el-Sissi  ni wenyeji  wa mkutano  huo  wa  siku  mbili  unaoahudhuriwa  na  viongozi 43 wa mataifa  54  ya  bara  hilo, ambapo  mataifa  mengine yanawakilishwa  na maafisa  waandamizi.

Putin amesema  biashara  inayofanywa na  Urusi  kwa  mwaka pamoja  na  mataifa  ya  Afrika  ilipanda  maradufu  katika  miaka mitano  iliyopita  na  kupindukia  dola  bilioni 20.

Amedokeza  kwamba, "ni wazi  kwamba  haitoshi" na  kuelezea nia yake  kwamba  biashara  hiyo  itaongezeka  tena  maradufu , "kwa wastani" katika  miaka  mingine  minne ama  mitano.

El-Sissi  amehimiza  makampuni  ya  Urusi  kupanua  uwekezaji  wao katika  bara  la  Afrika. "Kuna  fursa  muhimu  kwa  hilo  hivi  sasa," amesema.

Russland Afrika Gipfel
Wajumbe mbali mbali wakiwasili mjini Sochi kwa mkutano kati ya Urusi na AfrikaPicha: picture-alliance/dpa/V. Sharifulin

Urusi na  ushawishi katika Afrika

Urusi imefanyakazi  kwa  mbinu  sahihi katika  miaka  ya hivi  karibuni kupanua  ushawishi  wake  katika  bara  la  Afrika, ikichukua  fursa ya  kupungua  kwa  hamasa ya  Marekani  katika  bara  hilo  chini  ya utawala  wa  rais Donald Trump. Akichangia  katika  mjadala  kuhusu uhusiano  kati  ya  Afrika  na  Urusi rais  wa  Afrika  kusini Cyril Ramaphosa  alisema.

"Uhusiano wetu  haukuanza  jana. Ulikuwapo kwa  miaka  mingi na umekuwa  uhusiano uliotengenezwa  katika  mapambano. Na kwa njia  nyingi, Afrika  kusini, Afrika  kusini  iliyo huru,  iko  hivyo  leo kutokana  na  sababu ya  msaada tulioupata kutoka  kawa  watu wa Urusi."

Shirika  la  Urusi  la  uchunguzi wa  miamba na  ardhi  limetia  saini makubaliano  na  Sudan kusini , Rwanda na  Guinea kutafuta maliasili  za  mafuta  na  makaa ya  mawe. Putin pia  alikutana  na viongozi  kadhaa  wa  Afrika  kujadili kuhusu uwezekano  wa  miradi kadhaa.  Putin  alisema.

Südafrika Muhammadu Buhari und Cyril Ramaphosa
Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria (kushoto) na Cyril Ramaphosa (kulia9 wa Afrika kusini wamekutana tena mjini Sochi katika mkutano kati ya Urusi na Afrika.Picha: Reuters/S. Sibeko

"Urusi , kama  kiongozi wa  dunia  katika  nyanja ya  nishati ya nyuklia na uzalishaji wa  mafuta  ya  nyuklia, pamoja  na  Namibia, ambayo ni mtoaji  mkuu  wa  madini  ya  urani, zunaweza  kuanzisha ushirikiano  wa  karibu na  kuwa  washirika wazuri."

Putin amempongeza waziri mkuu  wa  Ethipia Abiy Ahmed kwa kushinda  tuzo ya  amani  ya  Nobel mapema  mwezi huu, akisifu juhudi  zake  za  kuleta  amani  na  nchi  hasimu  wa siku  nyingi Eritrea.