9 Februari 2021
Matangazo
Rais wa Zanzibar, Dokta Hussein Ali Mwinyi amesema hana wasiwasi wowote kuhusu majaliwa ya serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyoundwa hivi karibuni baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu ambao ulilalamikiwa na vyama vya upinzani. Sikiliza kipindi cha Kinagaubaga, ambapo mwandishi wa DW George Njogopa amefanya mahojiano maalum na Rais Mwinyi ambaye tayari ametimiza siku 100 madarakani. Mwinyi amedokeza matamanio yake kuhusu mwelekeo mpya wa kisiasa katika visiwa vya Zanzibar hasa baada ya kuundwa kwa serikali mpya ya Umoja wa Kitaifa inayovishirikisha vyama vya CCM na ACT-Wazalendo.