1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUganda

Raia wa Uganda wanapiga kura leo kumchagua Rais

15 Januari 2026

Raia zaidi ya milioni 21 wa Uganda wanapiga kura Alhamisi katika uchaguzi wa rais unaotarajiwa kuendeleza utawala wa muda mrefu wa Rais Yoweri Museveni.

https://p.dw.com/p/56pot
Uganda | Wagombea wakuu wa kiti cha Urais Yoweri Museveni na Bobi Wine
Picha za wagombea wakuu wawili wa kiti cha Urais nchini Uganda: Yoweri Museveni na Robert Kyagulani (Bobi Wine) mjini KampalaPicha: Sumy Sadurni/AFP

Museveni mwenye umri wa miaka 81 na aliye madarakani tangu mwaka 1986, anawania muhula wa saba, huku kukiwa na hofu kuhusu uwazi wa mchakato huo hasa wakati huu kukiwa kumezimwa mtandao wa intaneti na mawasiliano.

Hata hivyo, Museveni anakabiliwa na ushindani mkali  kutoka kwa mwanamuziki aliyegeuka mwanasiasa Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine, mwenye umri wa miaka 43, anayewakilisha kizazi kinachotamani mabadiliko ya kisiasa katika taifa la Afrika Mashariki lenye watu takribani milioni 45.

Wakati Uganda ikiingia kwenye uchaguzi wa rais, hatua za kuzima mtandao, kuwepo kwa wanajeshi mitaani na madai ya kuingiliwa kwa mchakato zimeibua maswali mazito kuhusu uwazi wa kura na mustakabali wa demokrasia.