1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uchaguzi wa Rais wafanyika Nigeria

Zainab Aziz
23 Februari 2019

Uchaguzi ulioahirishwa kwa wiki moja nchini Nigeria, utafanyika Jumamosi, lakini baadhi ya watu wanaona kwamba kujitokeza kwao vituoni ni kujiweka kwenye hatari ya kushambuliwa na kundi la Boko Haram.

https://p.dw.com/p/3DwLw
Kombobild Muhammadu Buhari und Atiku Abubakar

Rais Muhammadu Buhari amewataka wananchi wa Nigeria wajitokeze kwenda kupiga kura Jumamosi na ameahidi kwamba utakuwepo usalama wa kutosha. Katika uchaguzi huo ulioahirishwa wiki iliyopita Rais Buhari atapambana na mfanya biashara Atiku Abubakar ambaye hapo awali alikuwa makamu wa Rais. Tume huru ya uchaguzi nchini Nigeria wiki iliyopita iliahirisha uchaguzi huo wakati Wanigeria zaidi ya milioni 72 walipokuwa wanajitayarisha kwenda kupiga kura.

Akilihutubia taifa kwenye televisheni Rais Buhari amewataka Wanigeria wasiwe na wasiwasi na wawe na imani kwamba tume ya uchaguzi itatimiza jukumu lake. Naye mshindani wake kiongozi wa chama kikuu cha upinzani PDP Atiku Abubakar ametoa wito huo huo kwa wapiga kura.

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhar
Rais wa Nigeria Muhammadu BuhariPicha: DW/I. U. Jaalo

Zaidi ya Wanigeria milioni 84 wameandikishwa kupiga kura kwenye taifa hilo lenye wakaazi milioni 190 la magharibi mwa Afrika. Lakini kwenye maeneo mengi ya kaskazini, ambako uasi wa kundi la Boko Haram umesababisha vifo vya zaidi ya watu 27,000 na kuwafanya mamilioni kuyakimbia makazi yao. Maelfu ya watu huenda wasiweze kushiriki kwenye uchaguzi wa Jumamosi Februari 23.

Kwa Wakaskazini waliolazimika kuyakimbia makaazi yao kutokana na kushambuliwa mara kwa mara na kundi la kigaidi la  Boko Haram, hamu ya kupiga kura ni ndogo sana ingawa wanatarajia matokeo ya kura hiyo yatarudisha tena amani kwenye maeneo yaliyotawaliwa na matumizi ya nguvu.

Mwandishi: Zainab Aziz/RTRE

Mhariri: Grace Kabogo