1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Raia wa Mali waaza kupiga kura

28 Julai 2013

Raia wa Mali wanapiga kura leo Jumapili(28.07.2013) na kupuuzia vitisho vya waasi wa Kiislamu na kujitokeza kwa mamilioni kupiga kura kumchagua rais mpya ambaye anatarajiwa kuanzisha enzi mpya ya amani na uthabiti.

https://p.dw.com/p/19FKR
People line up to receive their voter identification cards in Senou June 29, 2013. Mali is scheduled to hold presidential elections on July 28. REUTERS/Adama Diarra (MALI - Tags: POLITICS ELECTIONS)
Wapiga kura wakijiandikisha nchini MaliPicha: Reuters

Wapiga kura watakuwa na fursa ya kuchagua miongoni mwa wagombea 27 wakati wakipiga kura kwa mara ya kwanza tangu mapinduzi ya mwaka jana katika nchi hiyo ambayo ni moja kati ya nchi za eneo hilo yenye demokrasia imara, baada ya wapiganaji wa Kiislamu walipochukua fursa ya vuguvugu la kutaka kujitenga na kudhibiti eneo kubwa la nchi hiyo upande wa kaskazini.

Uchaguzi umeanza saa nne asubuhi saa za Mali chini ya ulinzi mkali baada ya moja ya makundi ya Waislamu kaskazini ya Mali kusema jana Jumamosi (27.07.2013) kuwa litashambulia vituo vya kupigia kura.

Ousmane Alamine Toure holds up his NINA card, a recently introduced national identity card that will be used for the upcoming elections in Timbuktu on June 30, 2013. United Nations peacekeepers are preparing tomorrow to take over from African troops in Mali with a mission to ensure stability in the conflict-scarred nation just four weeks ahead of crucial elections. AFP PHOTO/SEBASTIEN RIEUSSEC (Photo credit should read Sebastien RIEUSSEC/AFP/Getty Images)
Matayarisho uchaguzi wa Mali raia akionesha kadi yakePicha: Sebastien RIEUSSEC/AFP/Getty Images

"Vituo vya kupigia kura na maeneo mengine yatakayofanyika zoezi hilo la kupiga kura katika kile wanachoita uchaguzi yatalengwa katika mashambulizi ya Mujahideen, " kundi la vuguvugu la umoja na Jihad katika Afrika magharibi (MUJAO) limesema katika taarifa iliyochapishwa na shirika la habari la Mauritania ANI.

Taarifa hiyo haikufafanua ni njia gani zitatumika katika mashambulizi hayo.

Kundi hilo limewaonya Waislamu wa Mali kutoshiriki katika zoezi hilo la kupiga kura , likiwaamuru "kujitenga na uchaguzi huo."

Licha ya kuwa kampeni iliyochukua wiki tatu ilimalizika rasmi Ijumaa bila kutokea tukio lolote baya , hali hiyo inasababisha kutanda kwa wingu la machafuko katika eneo la kaskazini ambalo limekuwa na shaka ya kuwapo tayari kwa Mali kufanya uchaguzi ambao utakuwa huru na wa haki na wenye kuaminika.

Wakosoaji wanasema

Wakosoaji nchini humo pamoja na nje ya nchi wamedai kuwa Mali, ikiwa chini ya mbinyo kutoka kwa jumuiya ya kimataifa , inaharakisha kufanya uchaguzi huo na kuhatarisha kuwa na uchaguzi ambao hautakamilika ambao unaweza kuleta madhara zaidi badala ya hali bora.

Lakini Louis Michel, mkuu wa kundi la uangalizi wa uchaguzi kutoka Umoja wa Ulaya, ameeleza matumaini siku ya Ijumaa, akisema hali ni nzuri kwa ajili ya kufanyika duru ya kwanza ya uchaguzi wa kuaminika.

"Naamini kwamba uchaguzi huu unaweza kufanyika katika muktadha na masharti ambayo yanakubalika na hayaruhusu hali ya kutoaminika ama udanganyifu wa matokeo," amewaambia waandishi habari katika mji mkuu Bamako.

Wasi wasi mkubwa kabla ya uchaguzi huo umekuwa ukielekezwa katika mji wa Kidal, uliokuwa ukidhibitiwa kwa muda wa miezi mitano na Watuareg wanaotaka kujitenga hadi pale makubaliano ya amani yaliporuhusu jeshi la Mali mapema mwezi huu kutoa huduma za usalama katika mji huo.

epa03179919 Mali parliamentary speaker Dioncounda Traore is sworn in as interim president during a ceremony in Bamako, Mali 12 April 2012. Reports state that the swearing in of parliamentary speaker Dioncounda Traore marks the return to civilian rule following the March 21 coup. The interim president is now tasked with organising elections within 40 days. EPA/STR
Kaimu rais wa Mali Dioncounda TraorePicha: picture-alliance/dpa

Mapigano kati ya Watuareg na raia weusi wenye asili ya Afrika kabla ya uchaguzi yamesababisha vifo vya watu wanne . Na watu wenye silaha wanaofikiriwa kuwa ni kutoka la National Movement for the Liberation of Azawad MNLA wamewateka nyara maafisa watano wa tume ya uchaguzi kilometa 200 kaskazini mwa Kidal.

Uchaguzi wa kwanza

Uchaguzi huo ni wa kwanza tangu jeshi kuasi Machi mwaka uliopita ambapo aliangushwa kutoka madarakani rais Amadou Toumani Toure ambaye alichaguliwa kidemokrasia. Mtafaruku uliofuatia ulisaidia kundi la MNLA, MUJAO na makundi mengine yenye mafungamano na al-Qaeda kulidhibiti eneo la kaskazini ya Mali.

A member of the Tuareg delegation takes part in a meeting on the Malian crisis on June 18, 2013 in Ouagadougou. The Malian government and Tuareg rebels occupying a key northern city signed an accord today paving the way for presidential elections in the west African state next month. Mali's territorial administration minister and representatives of two Tuareg movements signed the deal in Ouagadougou, capital of neighbouring Burkina Faso, as the lead mediator in negotiations, Burkinabe President Blaise Compaore, looked on. AFP PHOTO AHMED OUOBA (Photo credit should read AHMED OUOBA/AFP/Getty Images)
Makubaliano na makundi ya Watuareg yalitiwa saini mjini OuagadougouPicha: AHMED OUOBA/AFP/Getty Images

Katika mkesha wa uchaguzi , kaimu rais wa Mali Dioncounda Traore, katika hotuba aliyoitoa kuptia televisheni , amewataka watu wa Mali kuhakikisha kuwa wanajitokeza kwa wingi kupiga kura katika nchi hiyo ambayo watu wanaojitokeza kupiga kura kwa kawaida huwa chini ya asilimia 40. Traore binafsi si mmoja kati ya wagombea.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe

Mhariri: Sudi Mnette