1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin asitisha mapigano Ukraine kwa Pasaka ya Orthodox

Josephat Charo
10 Aprili 2026

Rais wa Urusi Vladimir Putin ametangaza kusitisha mapigano kwa muda katika vita vya Ukraine ili kuadhimisha Pasaka ya madhehebu ya Orthodox.

https://p.dw.com/p/5BwrS
Rais wa Urusi Vlaldimir Putin ametangaza kusitisha mapigano Ukraine kwa muda kwa ajili ya Pasaka ya Orthodox.
Rais wa Urusi Vlaldimir Putin ametangaza kusitisha mapigano Ukraine kwa muda kwa ajili ya Pasaka ya Orthodox.Picha: Alexander Zemlianichenko/AP Photo/picture alliance

Kremlin ilisema katika taarifa jana Alhamisi kwamba usitishaji huo wa mapigano unatarajiwa kuanza Jumamosi saa kumi jioni na kudumu hadi Jumapili nzima.

Hatua hiyo inakuja baada ya rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky kutoa wito mara kadhaa wa kusitisha mapigano wakati wa likizo. Wakristo wa Orthodox kama wale walio Urusi na Ukraine wanasherehekea Pasaka Aprili 12 mwaka huu.

Kremlin ilisema katika taarifa kwamba waziri wa ulinzi Andrei Belousov na mkuu wa wafanyakazi Valery Gerasimov waliamriwa kusimamisha shughuli zote za kijeshi wakati wa kusitisha mapigano kwa muda.

Taarifa hiyo pia ilisema wanajeshi lazima wabaki tayari kujibu uchochezi wowote kutoka kwa adui na  kwamba wanadhani upande wa Ukraine utafuata mfano wa Shirikisho la Urusi.