Polisi 5 wauwawa Irak
9 Septemba 2007Matangazo
BAGHDAD
Taarifa kutoka Baghdad,nchini Irak zinasema kwamba wapiganaji kadhaa waliokuwa na bunduki walihujumu kituo cha polisi katika kijiji kinachokaliwa mno na waumini wa madhehebu ya Sunni huko kaskazini mwa Irak hii leo na kuua askari 5 kabla hawakutimuliwa kwa msaada wa wakaazi wa huko.Washambulizi waliendesha mgari 10 kutoka magharibi mwa Irak hadi kwenye kijiji hicho cha Hajaj na kufyatua risasi katika kituo hicho cha polisi.