Pirlo aanza taaluma ya ukocha kwa ushindi
21 Septemba 2020Matangazo
Andrea Pirlo ameanza taaluma yake ya ukocha kwa ushindi baada ya Juventus kuanzisha kampeni ya kubeba taji la ligi la 10 mfululizo na ushindi wa 3 - 0 dhidi ya Sampdoria jana.
Pirlo amesema hataki kumuiga yeyote katika aina yake ya mchezo. Muitaliano huyo kiungo wa zamani wa Juve aliyepokea kibali chake cha ukocha wiki iliyopita, amewataja Pep Guardiola, Carlo Ancelotti na Antonio Conte. Amesema anataka kutumia mawazo yake binafsi na atachukua mfano kutoka kwa timu zilizomfurahisha.