1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Peshawar.Maafisa nchini Pakistan wailaumu serikali kwa shambulio la wanafunzi.

30 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CCxh

Waandamanaji na maofisa nchini Pakistan wameilaumu Marekani kwa mashambulizi ya anga hii leo ambayo jeshi lilidai limewauwa kiasi cha watu 80 wanaoshukiwa kuwa ni wanamgambo waliokuwepo katika kambi ya kigaidi.

Siraj-ul-Haq, naibu waziri kiongozi wa jimbo linaloongozwa na waislamu la Kaskazini Magharibi amejiuzulu baada ya kufanywa shambulio hilo katika shule ya kidini karibu na mpaka na Afghanistan.

Akielezea sababu za kujiuzulu kwake Siraj-al-Haq amesema ni kutokana na kuonyeshahuzuni zake dhidi ya shambulio lililouwa wanafunzi 80 wasio na hatia yoyote.

Siraj aliyehudhuria mazishi ya wanafunzi 20 kati ya waliouliwa hii leo katika Jimbo la Bajaur ameongeza kuwa, wengi wa waliouwawa ni watoto wadogo.