Outtara asema yuko tayari kuendelea kuhudumu kama rais
9 Januari 2025Matangazo
Katika hotuba yake kwa wanadiplomasia mjini Abidjan, Outtara mwenye umri wa miaka 83, ameeleza kuwa ana afya njema na mwenye hamu ya kuendelea kuwatumikia wananchi wa nchi yake.
Kiongozi huyo, aliyechaguliwa tena kwa muhula wa tatu katika uchaguzi uliozua utata mnamo mwaka 2020, hapo awali alionyesha utayari wa kustaafu, lakini akapendekeza kwamba washindani wake wazee pia wanapaswa kujiondoa kwenye siasa.